tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumanne, 6 Septemba 2016

tambua biashara isiyo halali

                                                                
Jinsi ya kutambua biashara za kimtandao zisizo halali(za kitapeli)


     Ajira ni tatizo kubwa linalokabili taifa na dunia kwa ujumla.Kila mara watu wanafikiria ni njia zipi mtu atazitumia kupata kipato kitakacho muwezesha kukidhi mahitaji yake pengine na familia yake.Jinsi gani ya kuongeza kiapato ndo swali gumu ambalo linahitaji majibu,je huyu mtu ameajiriwa au amejiajiri?.Vijana wengi wanaomaliza elimu zao wanafanya juu chini kujiwezesha na pengine kuajiriwa.Pamoja kwamba mtu amejiajiri au ameajiriwa bado kuna baadhi yao wanofanya biashara za kitapeli kama njia ya kujiongezea kipato.Pia idadi kubwa inajitokeza kwa watu ambao hawajabahatika kujiajiri au kuajiriwa.Baadhi ya watu wamepata pesa nyingi na pengine kutajirika kabisa kutokana na manbo ya kitapeli.Kitu kinachowafanya watu wafanye utapeli ni kutokana kwamba hii njia ya kujiingizia kipato isivyo halali haiitaji nguvu na pia ni rahisi kufanyika.Zipo dalili kadhaa zinazoweza kukupa ishara fulani juu ya biashara ambayo ni ya kitapeli.Dalili hizi zitakuwezesha kuhisi kuwa biashara hiyo ina viashiria vya kitapeli.Tuchambua dalili moja baada ya nyingine;




Mtu kutangaza biashara zake kupitia sehemu za kutolea maoni(comments)


      Kama wewe ni mtumiaji mzuri wa mitandao ya kijamii hususani facebook utakuwa umeliona au kukutana na  suala hili.Sehemu zenye maoni ndio mara nyingi kukuta matangazo ya aina hii.Matangazo hayo hotelewa bila yakujali kichwa cha habari cha mada husika.Kwa mfano sehemu watu walipotolea maoni kuhusu siasa ndipo mtu huweka tangazo lake la biashara ambalo haliendani kabisa na mada inayotolewa maoni.Lengo la mtu kuweka tangazo lake hapa ni kupata wateja wa huduma yake na siku zote mtu huangalia sehemu zenye maoni mengi ndipo huweka tangazo lake hilo.Ndiyo biashara yako inaweza kutangazwa sehemu ya kutolea maoni lakini je hilo tangazo lako linalingana na maoni hayo?.Endapo tangazo litatolewa kwenye maoni yahusuyo biashara tajwa basi hapo hamna tatizo.


     Kufanana kwa matangazo yanayotolewa


      Matangazo yanayotolewa hususani sehemu za kutolea maoni (comments) yana fanana fanana.Matangazo hayo ni kama mtu ameyanakili kutoka kwa mwingine.Maneno na mpangilio wakati mwingine hufanana kabisa na matangazo mengine kama hayo.Ukiyafuatilia hayo matangazo hayo kwa makini na kuyafananisha na matangazo maengine ambayo yamesha wahi kutolewa au umeyaona utangundua kuwa kuna ulinganifu fulani.Mwandishi huyo muda mwingine huchukua kila kitu kutoka katika tangazo jingine.Ukiataka kungundua hayo chukua matangazo mawili au matatu ambayo umeshawahi kuyaona na uyafananishe katika uandishi uliotumika katika matangazo hayo.Kufanana huku kunaweza kusiwe katika picha tu hata  video zilizotumika zinaweza  kufanana.Lakini mara nyingi maneno  huwa ndo yanafanana.



Tangazo kuahidi kupata pesa kwa muda mfupi




      Mara nyingi matangazo yanayotolewa na kumuahidi mtu kupata kiwango fulani cha pesa endapo atajiunga na biashara hiyo.Tangazo huelezea kwa kina jinsi utakavyoweza kupata pesa na kutajirika kwa kipindi kidogo tu  cha wakati.Tangazo hilo hutumia lugha ambayo itamuwezesha mtu kuamini kabisa juu ya kilicho zungumziwa hapo kuwa ni sahihi.Kwa mtu ambaye hajui utapeli juu ya matangazo hayo akiyapata kwa mara ya kwanza kuna uwezekano kabisa  wa kutumbukia katika mikono ya matapeli.Maana tangazo litamvutia mtu na kumpa hamasa ili tu aweze kupata pesa kwa muda mfupi kama tangazo lilivyo elezea.Hivyo basi inatupasa kuwa makini na matangazo yoyote yanayotolewa na kuyapima je ni ya kweli au siyo ya kweli.Ila dalili ya tangazo kukuahidi kupata kiwango kikubwa cha pesa kwa muda mfupi ni dalili ya utapeli.




       Kutotajwa kwa biashara yenyewe



      Hapa unakuta kwamba mtu anaizungumzia biashara yake lakini hakupi mwanga ni biashara ya aina gani.Huelezea kwa maneno mengi yenye kumvutia mtu kabisa kujiunga nayo.Katika maelezo atakayotoa hutokuta anakwambia ni biashara ya vitu gani au inafanyikaje.Kitu pekee baada ya kuelezea biashara yake atakuambia muwasiliane tu na kuacha taarifa zake za mawasiliano.Kabla ya kumtafuta mtu ni vizuri uwe na mwanga wa biashara aliyoitolea maelezo.Mtu huficha taarifa muhimu za biashara kama hiyo ili kuepuka kugundulika kama anafanya biashara ya kitapeli.Maana akitolea maelezo ya kukamilika hiyo biashara kwa mtu anaye fahamu basi ni rahisi kugundulika kuwa hiyo biashara ni ya kitapeli.Hivyo basi hii dalili ni ya muhimu kuichunguza kutokana na maelezo yatakayotolewa kuhusu biashara hiyo.




 Kutolea mifano ya watu                  waliofanikiwa kupitia biashara hiyo



      Mwisho kabisa matangazo hayo mengine hubeba mifano ya watu waliofanikiwa kupitia biashara hiyo.Wakati mwingine asipotaja watu waliofanikiwa nayo basi mwandishi yeye mwenywewe atasema amefanikiwa nayo kwa kiwango cha kutosha.Haya yote hufanyika ili kuongezea hamasa kwa mteja anayetakiwa kujiunga.Mtu akiona kumbe watu wanafanikiwa kupitia hiyo biashara basi ina kuwa ni rahisi naye kujiunga nayo.Je maelezo yote yatolewayo ni sahihi au yanaongezewa chumvi tu?.Hizi ni njia tu za kumshawishi mtu kujiunga na mara nyingi mifano itolewayo inakuwa siyo sahihi au imeongezewa chumvi kidogo.Usiamini asilimia mia(100%) juu ya taarifa zinazotolewa labda mpaka nawe uwe na ushahidi nazo.

Hizi ni dalili tu zinzoweza kuashiria biashara hiyo ni ya kitapeli na siyo kila biashara ikiwa na dalili moja kati ya hizi ni ya kitapeli.Hizi dalili zinakupa mwanga juu ya kutambua biashara za kitapeli.

Nini maoni yako kuhusu hili?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...