tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumapili, 4 Septemba 2016

biashara ya kimtandao

                          



            Njia pekee ya kumuwezesha mtu kupata kipato chake  mbali na kuajiriwa ni kuanziasha biashara yake binafsi au kujiajiri(ujasiriamali).Ajira ni changamoto kubwa, kwa kuwa wasomi wanaongezeka na fursa za ajira zipo zile zile.Kujiajiri kutamuwezesha mtu husasni kijana kupata kipato chake pasipo kumtegemea mtu mwingine amuajiri.Wazo linakuja ni biashara gani ya kufanya kumwezesha mtu kupata kipato chake binafsi?Je ni biashara gani yenye mtaji mdogo?Je hii biashara ya mtandao ni nini?
          Ujasiriamali ni uwezo wa kujiajiri .Unaweza ukawa na wazo zuri la biashara na ukaweza kuliendeleza wewe mwenyewe au pamoja na kikundi cha watu.Ujasiriamali unaweza kugawanywa katika mafungu mawili kutokana na fikra zangu;
  i.            Ujasiriamali wa kimtandao(biashara ya mtandao)
 ii.           
Ujasiriamali nje ya mtandao




              ujasiriamali wa kimtandao




       Hii ni biashara ambapo mtu anaifanya inayotumia chini ya asilimia hamsini za mtandao(50%).Aina hii ya biashara siyo kwamba mtu hatumii kabisa mtanado bali unakuwa chini ya asilima hamsini.Mfanyabiashara huyu anaweza kutumia mitandao ya kijamii au tovuti zinazofanya matangazo ya kibiashara.Ila muda mwingi anatumia kufanya biashara yake yeye mwenyewe.Mfano mfanyabiashara wa duka la nguo atatumia muda mwingi kuuuza bidhaa zake kwa wateja wake kuliko kuuza mtanandaoni.Vile vile anaweza kutumia fursa ya mtandao kutangaza biashara yake kufikia watu wengi zaidi.Pia katika biashara hii mfanyabiashara anaweza asitumie mtandao kabisa katika kufanya biashara yake ,mfano mkulima/mfanyabiashara asiyejua umuhimu wa mtandao.Mfanyabiashara wa aina hii ni wale wenye fikra kuwa mitandao ya kijamii siyo ya kutangaza biashara yake.Kutokuwa na mtandao hususani vijijini inachangia mfanyabiashara kufanya ujasiriamali wake nje ya mtandao.Ujasiriamali huu una faida zake ndo maana watu wanaendelea kuutumia,je hasara zake ni zipi?
             Mfanyabiashara nje ya mtandao hawezi akaongeza au kupanua soko la bidhaa zake.Hapa tunazungumzia kuongezeka kwa wateja wa huduma anazotoa mjasiriamali.Kutangaza biashara katika mitandao ya kijamii pamoja na tovuti kunasaidia kuongeza idadi ya wanunzi wa biashara yako.Hii inatokana na dhana kwamba idadi ya watu wanaotumia mtandao inaongezeka siku hadi siku.Uwezekano  wa kuapata wateja nje ya eneo lako ni mkubwa sana endapo mtando utautumia vizuri.
            Mfanyabiashara atashindwa kutoa  bei yenye ushindani ya bidhaa zake kutokana na ushindani uliopo.Kupitia mtandao itakuwezesha kujua bei za bidhaa kama zako zinazouzwa na wafanyanyabiashra wengine ndani na nje ya eneo lako.Kuangalia ubora wa bidhaa zinazozalishwa na watu wengine, hivyo kuweka bei kulingana na bei za wafanya biashara mwengine.Pasipo kujua hayo unaweza kuweka bei ya bidhaa yako ghali na bidhaa hiyo hiyo mafanyabiashara mwingine akaweka bei rahisi hivyo ukapoteza baadhi ya wateja.Japokuwa kitu cha kwanza cha kuangalia katika bidhaa yeyote ni ubora lakini bei pia ina umuhimu wake.


          

 
ujasiriamali nje ya kimtandao




      Hii ni biashara ambapo mfanyabishara anafanya shughuli zake zaidi ya asilimia hamsini(50%) mtandaoni.Ujasiriamali wa kimtandao ni moja kati ya biashara zenye mtaji mdogo kabisa.Hapa mfanyabiashara anaweza kuwa na sehemu mbili zinazoweza kumuingizia kipato kwa wakati maalumu.Kwanza kabisa ni sehemu/duka ambalo linauza bidhaa na sehemu ya pili ni mtandaoni.Oda za manuuzi ya huduma zinafanyika mtandaoni na wanuunuzi wanaenda kuchukua kwenye duka husika au wanapelekewa kwenye maeneo yao husika.Hivyo mjasiriamali anakuwa na vyanzo viwili ambavyo vinamletea wateja wa bidhaa zake kwa wakati.Biashara nyingi zinazo fanyika bila mtandao zitaanza kupungua wateja maana wafanyabiashara washaanza kutumia fursa bora ya mtandao kuongeza wateja .
         Hii ni fursa tosha kutokana na sababu kuwa gharama ya kutangaza biashara katika vyombo vya habari ni kubwa ukilinganisha na mtu atakaye tangaza biashara yake katika mtandao.Pia kupitia mtandao mfanyanyabiashara anaweza kufungua duka la kimtandao ambalo atauza bidhaa zake mwenyewe pasipo kuwa na duka halisi, hapa oda zote na manunuzi yanafanyika katika mtandao na mteja anapelekewa bidhaa alizonununa.Kupitia mtandao utangazaji wa bidhaa zako unawezekana ukawa bure kabisa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...