tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumanne, 13 Septemba 2016

FURSA KUTOKANA NA TOVUTI

                                                      
      Ni kweli kabisa kutokana na tovuti kuna fursa nyingi ambazo zinaweza kutengenezwa na kuwa biashara.Nafasi hizi zinatokana na matumizi ya mtandao katika jamii yetu.Vipengele vya kibiashara vinavyoweza kuanzishwa kutokana na uhifadhi na matumizi ya shughuli za kimtandao.Ujuzi wako wako, lengo lako na mtaji wako ndio njia pekee itakayokupa mwanga ni biashara gani ya kuchagua na kuifanyia kazi.Tanzania muamko wa biashara hizi bado upo chini sana hivyo ni nafasi ya pekee kuchangamkia nafasi hizi za kujiingizia kiapato.Udogo wa watu katika nyanja kama hizi unatokana na idadi ndogo ya watanzania wanaofanyia ujasiriamali kupitia mtandao.Endapo utakapo kusudia kuchukua sehemu mojawapo na kuifanyia kazi basi maendeleo kupitia kuongeza kipato yanaweza kufikiwa.Kitu cha msingi ni kuepuka kuanzisha biashara zitazokuwa zikihusishwa na masuala ya utapeli.Ukiepuka hili suala ni kufanya biashara yako ikue siku hadi siku.Tuangalie hizi fursa kutokana na tovuti;



Uhifadhi wa tovuti (web hosting).

       Hii ni biashara inayofanyika kwa kutunza au kuhifadhi tovuti.Sio kila kompyuta inaweza kuzitunza ni kupitia kompyuta maalumu (web servers) ndio tovuti hizi zinaweza kutunzwa .Vile vile unaweza kutunza tovuti yako kupitia kompyuta yako ya nyumabani.Gharama ya kuhifadhi tovuti ya mtu inatokana na kiwango cha nafasi na data atakazotumia vile vile maelewano na mtunzaji wa hizo tovuti.Biashara hii inahitaji uangalizi mkubwa sana  maana unatunza biashara za watu.Umeme wa uhakika unahitajika vile vile mtandao ambao lazima upatikane kwa asilimia mia moja na kwa mwaka mzima.Ina maana umeme ukikatika katika kompyuta unazotunzia basi na tovuti husika haitokuwa mtandaoni (haitopatikana ukiitafuta).Changamoto ya hapa ni wafanyakazi ambao watashughulikia mitambo (kompyuta) itakapokuwa na kasoro, umeme unaopatikana muda wote ,intaneti ya uhakika na kudhibiti uhalifu wa kimtandao katika kompyuta za kuhifadhia tovuti.Pamoja na hayo kama hauna vifaa hivi unaweza kupatana na makumpuni makubwa uwe kama mtu wa katikati (affiliate marketer) au muuzaji wa pili (reseller).Njia hizi mbili zinawezekana kama hauna mtaji wa kugharamia kompyuta za kuhifadhi tovuti(web servers).Ambapo utatoa huduma ya uhifadhi wa tovuti bila ya kuwa na wafanyakazi wala kompyuta za kutunzia tovuti.



Kuuza majina ya tovuti (domain names).

     Kila tovuti ina jina lake linaloitambulisha ikiwa mtanadoni.Kuna aina mbili za majina ya tovuti ,moja kuna yale yanayotumika kwa dunia nzima ambayo yanaishia na vifupisho kama com,net,org,xyz,design na mengine mengi.Aina ya pili ni majina yatumikayo na tovuti zilizo katika nchi husika kama yanayoishia na .tz kwa Tanzania au .ug kwa Uganda.Jina la tovuti yako linagharamiwa mwaka mpaka mwaka ambapo unaweza kuanzisha tovuti yako ambayo watu watakuwa wanalipia majina ya tovuti zao.Kwa majina haya yanayotumika dunia nzima ni vizuri ukawa muuzaji wa kati (affiliate marketer) au muuzaji wa pili (reseller) wa makampuni makubwa ambayo yanaendesha biashara hizi.Kwa majina yatumikayo nchini unaweza kuyauza mwenyewe kabisa ila kwa kufuta utaratibu maalumu uliowekwa.Hivyo basi kupitia kuuza majina haya ya tovuti unaweza kujiongezea kipato chako.



Utengenezaji wa tovuti (web design and development).

      Hapa inahitaji uwe na ujuzi wa baadhi ya lugha za kuprogramu tovuti kama vile html, php, javascript, css na nyingine nyingi.Vile vile kama hauna ujuzi huo zipo programu zitakazoweza kukusaidia kama adobe dreamweaver, microsoft expression web, adobe muse.Kama bado haujui kabisa jinsi ya kuandika lugha hizi za kuprogramu tovuti kuna programu nyingine ambazo zipo katika sehemu za uhifadhi wa tovuti (web hosting account) ambazo ni rahisi kutumia bila kuwa na ujuzi wa kuandika lugha za kuandika tovuti.Hizi ni kama vile wordpress, drupal, joomla, blogger na nyingine nyingi.Hivyo basi biashara hii inawezekana kwa mtu aliye na nia ya dhati kufanya hivyo na mwenye malengo nayo.Utakapoanzisha huduma yako hakikisha inatolewa kwa ubora wa hali ya juu ili kuwezesha kukuza jina la kazi yako.Ukishindwa kutoa huduma iliyo bora basi itakuwa ni vigumu kufanikisha malengo ambayo ulikuwa umejiwekea kuyakamilisha kwa muda fulani.



Huduma ya SEO.

    SEO ni kifupisho cha search engine optimization, ni huduma ambayo utawezesha tovuti ya mteja wako kuonekana kurasa ya kwanza kabisa katika programu za kutafuta kama vile google ,yahoo na bing .Tovuti yako inapoonekana katika kurasa ya kwanza ya hizi programu inakuwa ni rahisi kabisa kupata watembeleaji katika tovuti yako.Lengo kubwa la kufungua tovuti ni kuhakikisha inaonekana kwa watu wengi na walengwa wa suala hilo.Ili kuhakikisha inaonekana katika kurasa ya kwanza kabisa katika programu hizi za kutafuta huna budi kuhakikisha tovuti yako inakidhi viwango vinavyotakiwa vya seo.Bila ya kufuata viwango hivi tovuti yako haitoweza kuonekana katika kurasa za kwanza hivyo inaweza  kusababisha ukakosa wateja au ukapunguza wateja kakia ujasiriamali wako.Hapa unaweza kupata ajira kwa kutoa huduma hii kwa watu ambao wanaohitaji.Ukiwa na ujuzi katika sula hili utaweza kujiongezea kipato kupitia huduma ya seo.Epuka njia zisizo sahihi (black hat) katika kutoa huduma yako kwa wateja.



Toa ushauri katika kuitangaza tovuti.

    Mtu anaweza kuanzisha tovuti ila suala ya kuitangaza likiawa ni jukumu zito sana. Hapa kama una ujuzi kuhusu hili huu ndo wakati muafaka wa kuongeza kipato chako.Ushauri kama wa biashara katika mitandao  ni muhimu sana katika kukuza  tovuti yako.Jinsi gani uendeshe biashara yako kupitia tovuti,je ni njia gani utumie kuitangaza biashara yako?. Mtu utumie matangazo ya kulipia (paid ads), kupitia mitandao ya kijaamii (social media marketing) au utumie seo (search engine optimization) tu.Vile vile katika kufanya mauzo ya bidhaa zako utumie njia gani ambazo zitakidhi matakwa ya watumiaji.Pande hizi mbili ni muhimu kuzingatiwa kuwezesha kukuza kipato cha tovuti yako.Kama una ujuzi wa mambo kama haya ni rahisi kuongeza mapato yako kupita watu watakaotaka huduma kama hizi.Hivyo ushauri kupitia kuitangaza tovuti unaweza kukuwezesha kupata ajira pia.



Una maoni gani? Andika katika kisanduku cha maoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...