tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumapili, 11 Septemba 2016

wizi wa mtandao tanzania

                            
          Sayansi na teknolojia ni jambo muhimu sana katika kukua kwa uchumi wa nchi yoyote ile.Maana teknolojia itawezesha kubuni mifumo ambayo itasaidia watu kufanya kazi kwa ufanisi na kwa muda mdogo.Teknolojia katika mifumo ihusiyo miamala ya  kipesa ikiwa ndogo ndio chanzo kikubwa cha kuanzisha wizi wa mtandaoa.Watu wenye ujuzi hutumia mianya katika mifumo hiyo kufanya matukio ambayo yanaweza kusababisha upotevu wa pesa.Haya yote yanatokana na kwamba teknolojia itumikayo katika hizi kampuni zenye miamala ya kipesa ni ndogo sana.Vile vile makampuni haya yanawezekana yasiwe na wataalamu wenye ujuzi wa  kutosha katika kutimiza majukumu yao, au kampuni lina miundombinu isiyokidhi usalama wa pesa zilizowekwa.Vilevile inawezekana baadhi ya wafanyakazi ndo wahalifu wenyewe au wanashirikiana na wahalifu hao maana yote haya yanawezekana.Hivyo makampuni hayo hayana budi kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na suala hili.



           
Wizi katika mitandao ya simu


      Hili suala la wizi katika mitandao ya simu Tanzania linaonekana kukua siku hadi siku.Ambapo mtu anachukua namba za simu za watu pengine mnaoheshimina nao na kukutumia ujumbe mfupi ambao utakutaka utume pesa kiwango fulani ila atakurudishia  kwa muda ambao atautaja yeye.Je hizi namba wanazipataje?.Hizi namba zinaweza kupatikana kutokana labda mtu ameibiwa simu yake au ameiangusha.Vile vile mtu anaweza kukupigia na kujifanya ni mtoa huduma katika mtandao wako wa simu  na kuanza kukuuliza maswali mengi yahusiyo simu yako.Maswali haya yanaweza kuwa matumizi yako ya miamala ya pesa katika simu yako, tarehe ya mwisho ya muamala, tarehe ya kuzaliwa na pengine hata namba yako ya siri.Ila namba itakayokupigia hapo mara nyingi siyo ya huduma kwa wateja( mfano 100 kwa Vodacom) bali ni namba ya kawaida tu kama za watu wengine unaowasiliana nao.Mtu akipata taarifa kama hizi anaweza kuibadilisha laini yako na kuanza kuitumia yeye mwenyewe ,ambapo anaweza kutoa pesa iliyo kuwepo au kuanza kuwatumia ujumbe watu wamtumie pesa kwa hiyo namba.Hapo namba yako ikibadilishwa, mtandoa  hautosoma katika laini yako na itakuwa imefungiwa.Tuzingatie haya yafuatayo kuepuka wizi;


   
Pindi simu yako inapopotea (kuibiwa au kudondoshwa) toa taarifa polisi vile vile wasiliana na huduma kwa wateja waifunge   mpaka    hapo   utakapoirudisha tena au kuisajili upywa (renew).


   
 
Hakikisha unapowasiliana na huduma kwa wateja basi hiyo namba unayowasilina nayo iwe inajulikana na watu pia na mtandao husika umeitoa itumike kwa huduma kwa wateja .Vocha za mitandao mara nyingi huwa zinakuja na namba za huduma kwa wateja ambazo unaweza kuzitumia pia.



Usimwambie mtu taarifa zako za siri zihusiyo miamala yako au laini yako kwa ujumla.


  
Mtu akikutumia ujumbe mfupi wa kutaka pesa basi mpigie uhakikishe kuwa ni yeye kweli vile vile kama ana laini zaidi ya moja mpigie kwa laini nyingine  uwe na uhakika zaidi.

 
Wekea nywila simu yako (passwords).

Usitunze taarifa za siri katika laini yako kwa muda mrefu.Mfano ujumbe mfupi utakaotumiwa na mtandao kuhusu kubadilisha nywila zako (passwords).
                           

               
WIZI MTANDAONI (INTERNET)


    Wizi kupitia mitandao pia unaweza kufanyika kupitia taarifa tunazozitoa  kwa watu wasio waaminifu.Hapa wizi huu unafanyika mara nyingi mtu unapofanya manunuzi  au kulipia huduma fulani mtandaoni, ambapo utatakiwa kuandika taarifa muhimu kuhusu akaunti yako ya benki.Wizi wa ana hii unaweza kufanyika kwa njia mbili moja ni kupitia kufanya manunuzi katika tovuti zisizo aminika.Hakikisha unapofanya manunuzi, katika tovuti unayofanyia manunuzi au kupata huduma fulani inatambulika vizuri.Maana ukifanya miamala yako katilka tovuti hizi zisizo aminika unaweza kupoteza pesa zote zilizo katika akaunti yako.Njia ya pili inafanyika kupitia kurasa zisizo halali za tovuti husika.Unaweza kufanya miamala katika tovuti husika kumbe ile kurasa unayotumia imebadilishwa bila ya wewe kujua.Hii inawezekana endapo utaambiwa kufanya muamala kupitia linki utakayotumiwa kupitia barua pepe au ujumbe mfupi.Tufanye haya kusaidia kuepuka kupoteza fedha zetu;

  i.    Unapofanya miamala katika tovuti hakikisha hizo tovuti zinaaminika(trusted sites).

  ii.   Kuwa makini na miamala unayotakiwa kuilipia kupitia linki za barua pepe au ujumbe mfupi.


   iiiUsindike namba yako ya siri katika tovuti unazo takiwa kufanya miamala.




Andika maoni yako kuhusu hili katika kisanduku cha maoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...