tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumapili, 11 Septemba 2016

Namna ya kuongeza kipato

                          

      Pamoja na kuwa na kazi ya kufanya au kutokuwa nayo inawezekana hauna kipato cha kutosha kitakacho kuwezesha kukidhi mahitaji yako.Kipato chako ndicho kitakuwezesha kufanya shughuli zako za kimaendeleo ndani na nje ya familia yako.Kipato cha kutosha kitakuwezesha kumudu mahitaji ya familia na kufanya shuguli za maendeleo.Endapo kipato chako kitatumika kukidhi mahitaji ya familia tu bila kufanya shughuli za kimaendeleo basi unahitaji kuongeza kipato chako.Kuongeza kipato kutakuwezesha kuendelea mbele na kutotegemea mshahara pindi unapomaliza kazi( kustaafu).
   Zipo njia za kuongeza kipato kupitia mtandao ambazo mtu anaweza kuzitumia na kufanikisha kuongeza kipato chake .Kitu cha msingi ni kuangalia njia ambazo ni za ukweli na hazina utapeli wowote.Uzuri wa baadhi ya njia hizi zinazoweza kutumika katika kuongeza kipato ni kwamba unaweza kuzifanya mbali na muda wa kazi.Njia hizi zinafanya kazi kwa ajili yako ukiwa katika shughuli zako za kawaida.



           
NJIA ZA KUONGEZA KIPATO



Fungua tovuti (website) kwa ajili ya biashara yako.


    Idadi ya watu wanaotumia mtandao Tanzania inaongezeka siku hadi siku.Hivyo basi hii ni fursa pekee itakayo muwezesha mtu kukuza kipato chake binafsi.Kama una biashara yako na ungependa kuongeza idadi ya  watumiaji wa bidhaa zako basi njia bora zaidi ni kufungua tovuti kwa ajili ya biashara yako.Biashara zinazo fanyika mtandaoni zina asilimia kubwa ya  kufanikiwa kuliko zile zisizo tumia mtandao.Utakapo fungua tovuti yako hapo utakuwa na vyanzo vya wateja vya ania mbili,moja ni wale wateja wa kawaida ambao hawatumiii mtandao na aina ya pili ya wateja ni ya wale wanaotumia mtandao kutafuta bidhaa za kununua. Hivyo idadi ya wateja katika biashara yako itaongezeka.



Tangaza biashara yako katika tovuti za matangazo (classified ads  websites).


     Kupitia tovuti zinazotoa huduma ya kuweka matangazo yako ya biashara  bure  kama vile kupatana.com na nyingine nyingi ambazo unaweza kutangaza biashara yako.Tovuti hizi zitakusaidia katika kuongeza iadadi ya wateja katika biashara yako.Huduma kama hizi anaweza kuzitumia mtu ambaye ana tovuti yake ya biashara  pia ambaye hajafungua tovuti kwa ajili ya biashara yake.Ukiweka biashara yako katika tovuti hizi basi kuna uwezekano mkubwa wa kuongeza mauzo kwa ajili ya biashara yako.Ambapo mtu atafanya manunuzi na malipo yatafanyika kutokana na utaratibu wa tovuti husika.


Anzisha tovuti ya matangazo ya kibiashara (classified ads website).


  Njia nyingine inayoweza kukuongezea kipato ni kufungua tovuti za kibishara ambapo mtu unaweza pia kutangaza biashara yako.Lengo kuu la kuanzisha  tovuti za kibiashara ni kuwezesha watu kuweka matangazo yao katika mtandao kiurahisi na kwa muda mfupi.Inakuwa rahisi watu kutafuta bidhaa wanazo zihitaji  katika hizi tovuti maana watazipata kiurahisi na kuwezesha kulinganisha na bidhaa nyinginezo zilizowekwa katika mtandao.Kitu cha msingi ni kuwezesha biashara yako kutambulika kiurahisi na watu wengi hivyo kufanya wepesi wa kuitumia.Hapa mtu anaweza kuongeza kipato kwa kutangaza baadhi ya matangazo kwa malipo maalumu kutokana na makubaliano na wateja wake.Watu wengi wanatumia matangazo yaliyodhaminiwa (sponsored/premium ads) katika kuingizia kipato tovuti zao.                    
                                                                                    

  Changamoto inakuja ni jinsi gani ya kuanzisha hizi tovuti.Je ni kiwango gani cha pesa unaweza kukiweka katika kuanzisha mradi wako.Ukweli ni kwamba kiasi cha pesa ambacho utakiweka hapa kinatokana ana aina ya tovuti uitakayo kuianzisha.Kufungua tovuti kama ya matangazo ya kibiashara ni gharama kidogo ukilinganisha na tovuti za kawaida .Maana katika tovuti hizi kiwango kikubwa cha nafasi kinahitajika kutunza tovuti yako.Gharama hii utakayo ilipia  ni ndogo kuliko kodi ya chumba chako cha biashara kwa mwezi mmoja.Pesa hii utayo lipia hapa itakuwezesha kuendesha tovuti yako kwa mwaka mzima.Lakini tovuti za kawaida gharama yake nia ndogo ambayo kila mtu anaweza kuimudu na kuanzisha tovuti yake.Haihitaji uwe na ujuzi na lugha za kompyuta kuweza kufanikisha hili,  kuna programu ambazo zipo tayari kabisa kuwasaidia watu wasiojua lugha hizi za kompyuta kutengeneza tovuti zao.
  Una maoni/ushauri kuhusu hili au unahitaji maoni/ushauri kuhusu hili suala basi andika lolote katika kisanduku cha maoni vile vile jiunge(subscribe) kupata taarifa pindi tunapoandika makala.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...