tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumanne, 13 Septemba 2016

JINSI YA KUANZISHA BIASHARA

                      

     Ni kweli kabisa kwamba njia moja wapo itakayokuwezesha kuanzisha biashara yako ni mtandao.Fananisha mtandao kama ni shamba  kubwa ambapo mtu unaweza kulima mazao yako, na tovuti ni kama mmea utakaokuwezesha kuvuna matunda yako (kipato).Utakapotunza mmea wako vizuri ndio utakapopata mazao yenye ubora.Kufungua tovuti ndio njia pekee itakayokuwezesha kuendesha biashara yako au huduma zako na pengine kukuingizia pesa .Hiyo utakapokuwa na tovuti mtandaoni basi ni lazima uifanye kama kitegauchumi kitakacho kuingizia kipato.Ijapokuwa kufungua tovuti au kufanya biashara ya mtandaoni ni rahisi lakini kuna changamoto zake.Ni biashara ya aina gani unataka uianzishe ,walengwa wake ni akina nani, bidhaa gani unataka uwauzie,njia zipi za kuwasambazia?. Vitu kama hivi ni muhimu kuvijua ili kuweza kufungua tovuti kwa ajili ya biashara yako.
     Sio lazima unapofungua tovuti iweze kukuingizia kipato.Hapa inatokana na lengo lako wewe unafungia kutimiza matakwa gani.Tovuti zisizo ingiza kipato mara nyingi ni tovuti za kutoa taarifa/habari kwa jamii kama tovuti za shule na vyuo.Lakini kumbuka mtandao ni soko kubwa linalokua siku hadi siku hivyo linaweza kutumika kama njia mojawapo ya kukutafutia wateja.Mbinu na mikakati madhubuti ndiyo jambo la msingi katika kufungua biashara yako ya mtandao.Utakapofungua tovuti bila ya kujua ni kitu gani unataka ukiweke ,itakuwa ni vigumu kutengeneza kipato chako.Hivyo basi ni njia gani zitakazo kuwezesha kufungua tovuti yenye mafanikaio?.Fuatilia lengo moja baada ya linguine katika Makala hii;



Uwe na kitu adimu na chenye thamani kuwapa /kuwauzia watu.

    Je una kipaji,biashara au huduma ambayo ni nzuri na watu wanaihitaji?. Hapo ndipo uanzishe tovuti yako kwa ajili ya hiyo huduma au biashara.Watu siku zote wanahitaji kupata huduma iliyo bora na isiyo na mashaka yoyote.Utakapoanzisha biashara yenye thamani itakuwezesha kupata wateja wengi na kwa haraka zaidi.Fikiria kitu ambacho watu wanakifikiria kukipata kutoka katika huduma fulani na hawakipati, hapo ndio uanzishe huduma kwa ajili ya kitu hicho watu wasichokipata.Vile vile ubora wa biashara yako au huduma yako uwe na kiwango kikubwa.Utakapouza au kutoa huduma yenye ubora basi biashara yako au huduma yako itadumu kwa muda mrefu zaidi.Hii ndio sehemu ya muhimu kabisa maana watu wanapenda kuona vitu vipya na vyenye ubunifu ndani yake.Ukifanikiwa katika sehemu hii ya kwanza ya kutambua huduma au biashara ya kuwauzia watu sehemu zinazobaki zinakuwa ni nyepesi kufanyika.



Fungua tovuti kwa ajili ya hiyo huduma/biashara.

    Ukishakuwa na wazo au lengo lako toka hapo awali ndipo sehemu hii ya pili inafuata.Baada ya kutafakari huduma bora ya kuwapa watu ndipo unapoyaweka mawazo yako katika vitendo.Fungua tovuti kwa ajili ya wazo lako na yenye mvuto kuwavutia wateja wako.Unaweza kuibuni tovuti yako wewe mwenyewe au ukamlipa mtu kiwango fulani cha pesa mtakacho kubaliana ili aweze kukubunia tovuti yako.Pia unaweza kuibuni wewe mwenyewe maana kuna programu ambazo zinaweza kukusaidia kubuni tovuti yako bila kuwa na utaalamu  wa lugha za kompyuta.Chaguo ni lako ila lengo ni kuwezesha wateja wako wapate huduma nzuri na bora ambayo hawaipati sehemu yoyote ila katika tovuti yako tu.Tovuti yako lazima iweze kuangalika kiurahisi katika simu na vile vile kompyuta.



Tangaza biashara yako/huduma.

      Hiki ni kipengele cha mwisho kabisa katika kuhakikisha biashara yako inafanikiwa.Lazima utangaze biashara yako ili uweze kupata wateja wengi siku hadi siku.Matangazo ya biashara yako yatakuwezesha kujua changamoto zilizopo katika hiyo biashara uliyoianzisha.Unapotangaza biashara yako tunazungumzia kutangaza tovuti yako.Njia zipi utakazotumia kutangaza tovuti yako au kuongeza wateja.Ukiitangaza tovuti yako itakuwezesha kujulikana kiurahisi kwa watu wenye mahitaji ya huduma yako.Tangaza kupitia mitandao ya kijaamii vile vile itasaidia kuongeza idadi ya watembeleaji wa kwenye tovuti yakio.Usipotumia mbinu sahihi katika kutangaza tovuti yako  basi itakuwa ni vigumu katika kukamilisha malengo yako.Hili suala sio la kutilia shaka sana endapo unatoa huduma iliyo na ubora ambao kila mtu anauhitaji.Utakapo toa huduma iliyo bora basi itakuwa ni rahisi kuongeza idadi ya wateja maana watu wanatafuta huduma yako iliyo bora sana kuliko nyingine.




Unafikiria nini kuhusu kuanzisha biashara ya kimtandao ,andika maoni yako katika kisanduku cha maoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...