tangazo

Uza/Nunua mifugo na vifaa vya ufugaji kuptia Mfugaji Marketplace

Jumatatu, 5 Septemba 2016

utapeli na biashara ya mtandao

                 


         Je utapeli unafanyika mitaani tu au hadi mtandaoni ? ………..jibu ni NDIYO, je ni kivipi?.Basi fuatilia Makala hii kwa undani ufahamu utapeli unavyofanyika .Utapeli huu unafanyika kupitia mawazo ya kawaida ya biashara.Makampuni mengi huwa yakimtamanisha mtu njia ambazo atazitumia na kupata peasa kwa haraka zaidi.Hapo ndipo mtu hujikuta ametumbukia katika mikono ya matapeli.Utapeli katika mtandao unashika kasi siku hadi siku.Makala hii itazungumzia aina moja ya  utapeli unaofanyika katika matandao hususani Tanzania.Hii itakuwezesha kuchukua njia thabiti za kuepukana nao vilevile kushauri wengine kuhusu suala hili.



      MAKAMPUNI YA UTAPELI KUPITIA MTANDAO


         Je kuna makampuni nchini yanayofanya utapeli bila ya serikali kujua au wananchi wake? 


    Kuna makampuni nchini yanafanya utapeli na pengine wanaojiunga hawajui kuwa ni utapeli tu.Makampuni ya aina hii nchi nyingi yameshapigwa marufuku na serikali za nchi husika.kampuni la kitapeli utaligundua kwa ishara kuu moja ,hayana bidhaa za kuuuza.Makampuni haya huwataka watu wajiunge kwa kiwango fulani cha pesa, na kila mtu yoyote atakayeunganishwa na mteja , mteja huyo atapata kiwango fulani cha pesa.Mara nyingi makampuni kama haya hutumia maneno tu kumshawishi mteja wao,kwa kila unapoongeza mtu katika huo mtandao basi pesa yako ndiyo inavyoongezeka.
      Kampuni kama forever living products siyo la kitapeli maana wana bidhaa zao zinazo julikana na zipo wazi kabisa.Japokuwa pia unaweza kupata kiwango fulani cha pesa unapoongeza mtu katika mtandao ila bado sio la kitapeli kabisa.Kama ungependa kufanya biashara na hii  kampuni ,basi jiunge nalo maana siyo la kitapeli.Tafuta mtu unayemjua ambaye yupo katika kampuni hii akupe ushauri zaidi namna ya kujiunga kama utapendelea.Kampuni jingine linalofanana na hili ni trevo nalo si la kitapeli.Jinsi biashara inavyoendeshwa na kampuni la forever living products inafanana na kampuni la trevo. Jiunge na makampuni haya kama utapendelea .Ila uwe unajua jinsi ya kufanya biashara(elimu ya biashara), maana kuwa na biashara na kufanya biashara ni vitu viwili tofauti kabisa.Pasipo elimu muhimu ya biashara basi hutoweza kuiendesha biashra yako na itakosa wateja.
  Makampuni tunayozungumzia kuwa ni ya kitapeli ni yale ambayo hayana bidhaa ya kuuza.Unajiunga kwa kiwango fulani na kila utakaye muunganisha basi nawe utapata asilimia fulani kutokana na huyo mtu uliye muunganisha.Inamaana ukijiunga ukakosa mtu wa kumuunga inamaanisha hela uliyotoa imeenda bure, huu ni utapeli.Fikiria kwa mfano mtandao ni wa watu wa nchini tu, na watu wote wakajiunga je huo mtandao  utaendelea kukua?. Hii inamaanisha watu wasipojiunga basi na mtandao wote utapotea kabisa na kufa.Mtandao ukifa na pesa yako imeenda na hakuna sharia ya kukuklinda wewe uliyejiunga.Kupitia maelezo niliyoyatoa basi unaweza kutambua ipi ni kampuni ya kitapeli na ipi siyo ya kitapeli.
     Kabla ya kujiunga na kampuni yoyote inakubidi ufanye uchunguzi wa kina kuhusu hiyo kampuni. Je ina tambulikas na serikali? Ina bidhaa ya kuuza? Inafanyaje biashara yake?. Uchunguzi utakuwezesha  kupata kampuni nzuri ambayo inaweza kukuongezea kipato chako.Epuka makampuni yanayokuahidi kiwango kikubwa cha pesa utakapo jiunga, hii huwa ni kivutio kupata wateja wengi.
     Makala hii fupi imeandikwa kukupa muongozo na sio kukushawishi ujiunge na makampuni tajwa hapo juu.Hii ni kukuelewesha  makampuni ya kitapeli na yasiyo ya kitapeli endapo ukitaka kufanya biashara nayo.Hivyo basi natumaini utakuwa umepata muongozo mzuri juu ya makampuni hayo, kwa lolote basi usisahau kuandika maoni yako hapo chini.

   

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kufanya biashara ya samaki aina ya Degere

  1. Ufafanuzi Samaki aina ya degere ni sangara ambao wanakuwa na ukubwa ulio pungufu ya sentimeta 48 ambazo ndio ukubwa unaokubalika kisher...